BMH KUJENGEWA KITUO CHA UMAHIRI CHA UPANDIKIZAJI ULOTO EAC
BMH KUJENGEWA KITUO CHA UMAHIRI CHA UPANDIKIZAJI ULOTO EAC

Hospitali Benjamin Mkapa (BMH) itajengewa Kituo cha Umahiri cha Upandikizaji Uloto cha Jumuiya ya Afrika Mashariki  (EAC), kwa mujibu wa Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu.

Wakati akiwasilisha bajeti ya Wizara ya Afya kwa Mwaka wa Fedha 2024-2025, Waziri Mhe. Ummy, amesema BMH imechaguliwa na EAC kwa kuwa ni Hospitali pekee katika Ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati kutoa huduma hii muhimu afya.

"Napenda kumpongeza Dkt. Alphonce Chandika, Mkurugenzi Mtendaji kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa na timu yake," amesema Mhe. Waziri. 

Upandikizaji uloto ni matibabu yanayotolewa na BMH kutibu siko seli. Huduma hii imezinduliwa Mei, 2023.

Mpaka sasa, watoto 10 waliokuwa na siko seli wameishapandikizwa uloto  katika Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH), huku vipimo vikiwa vimethibitisha kuwa watoto wanne wa kwanza waliotimiza mwaka mmoja toka kupata kupata matibabu hiyo wamepona ugonjwa huo.

Dondoo za Afya na Habari
Kula Mlo Kamili
Kula Mlo Kamili

Eat a combination of different foods, including fruit, vegetables, legumes, nuts and whole grains. A...

  View more
Usivute Sigara
Usivute Sigara

Uvutaji wa sigara ni hatari kwa afya ya mapafu yako, uvutaji wa sigara unaweza sababisha matatizo ya...

  View more
Punguza Vyakula vyenye mafuta mafuta
Punguza Vyakula vyenye mafuta mafuta

Fats consumed should be less than 30% of your total energy intake. This will help prevent unhealthy...

  View more
Kuendesha Gari.
Kuendesha Gari.

Unashauriwa kutokuendesha gari kila siku na wakati mwingine unatakiwa kutembea walau miguu yako na m...

  View more
Epuka ulevi wa Pombe
Epuka ulevi wa Pombe

There is no safe level for drinking alcohol. Consuming alcohol can lead to health problems such...

  View more