Idara ya Ustawi wa Jamii

Published: Sep 10, 2025
Idara ya Ustawi wa Jamii cover image

Utangulizi:

Idara ya Ustawi wa Jamii ni kati ya idara ndani ya Hospitali ya Benjamin Mkapa. Idara inatoa huduma za Amara Jamii (Social Work) ambazo ndio msingi mkuu wa huduma za Ustawi wa Jamii katika mahitaji mbali mbali na maeneo ya huduma za matibabu tofauti. Kazi kuu ya wataalamu wa Amara Jamii (Social workers) ni kusaidia Wagonjwa na familia zao au wateja kuweza kumudu athari zitokanazo na ugonjwa /magonjwa wakati wa matibabu na jinsi ya kuishi baada ya mabadiliko ya kiafya. Miongoni mwa huduma kuu zaidi katika idara ni pamoja na; 

• Tathmini ya hali ya Kisaikolojia kwa wagonjwa na familia zao

• Unasihi na Tiba saikologia (Counseling & Psychotherapy):

• Elimu kwa Wagonjwa na Familia:

• Ushauri wa rasilimali na mpango wa kurudisha wagonjwa nyumbani baada ya matibabu (Resource Counseling and Discharge Planning):

• Msaada kwa wagonjwa wa nje (Supportive Care to Outpatients):

 • Huduma za malalamiko (Complaints Services)

Huduma za Ustawi wa Jamii zilizofikiwa na Mafanikio yake:

MWAKA

Kusikiliza na kutambua mahitaji ya wagonjwa/wateja

Hafua za msaada na tiba  saikolojia  kwa wagonjwa/ wateja na familia zao

Malalamiko yaliyopokelewa na kutatuliwa

Wagonjwa waliopatiwa msaada wa matibabu

2021/2022

12,000

754

35

2,181

2022/2023

11,622

665

38

2,652

2023/2024

12,877

908

44

2,234

2024/2025 Machi

9,412

868

39

1,811

Jumla kuu

45,911

3,195

156

8,878