BMH YAPELEKA HUDUMA ZA DHARURA KATESHI
BMH YAPELEKA HUDUMA ZA DHARURA KATESHI

Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) imepeleka timu ya wataalamu katika mji wa Katesh kuongeza nguvu za huduma za Kiafya za dharura kwa manusura wa Mafuriko na Maporomoko ya aridhi yaliyosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha.

Dkt. George Dilunga, Bingwa wa Magonjwa ya Dharura na Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Dharura BMH ameongoza timu ya Madaktari na Wauguzi kuelekea Kateshi, Hanang Mkoani Manyara mapema leo.

“Tunakwenda kuhakikisha tunatoa msaada wa huduma za dharura kwa manusura, pamoja na sisi tumebeba vifaa vitakavyohitajika, zikiwemo dawa za aina mbalimbali zinazohitajika katika dharura ya namna hiyo” Amesema Dkt. Dilunga.

Disemba 4, Mheshimiwa Dkt. Godwin Molleli, Naibu Waziri wa Afya alitoa taarifa ya huduma za Afya huko Kateshi, pamoja na mambo mengine alitaja utayari wa Wizara kutoa huduma za Afya ambapo majeruhi 93 walikuwa wakipokea huduma katika hospitali na vituo mbalimbali vya Afya.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Manyara Dkt. Queen Sendiga, hadi kufikia asubuhi ya leo, watu 63 wamethibitika kupoteza Maisha kutokana na athari za mafuriko na maporomoko ya aridhi yaliyotokea mwishoni mwa wiki.

Dondoo za Afya na Habari
Kula Mlo Kamili
Kula Mlo Kamili

Eat a combination of different foods, including fruit, vegetables, legumes, nuts and whole grains. A...

  View more
Usivute Sigara
Usivute Sigara

Uvutaji wa sigara ni hatari kwa afya ya mapafu yako, uvutaji wa sigara unaweza sababisha matatizo ya...

  View more
Punguza Vyakula vyenye mafuta mafuta
Punguza Vyakula vyenye mafuta mafuta

Fats consumed should be less than 30% of your total energy intake. This will help prevent unhealthy...

  View more
Kuendesha Gari.
Kuendesha Gari.

Unashauriwa kutokuendesha gari kila siku na wakati mwingine unatakiwa kutembea walau miguu yako na m...

  View more
Epuka ulevi wa Pombe
Epuka ulevi wa Pombe

There is no safe level for drinking alcohol. Consuming alcohol can lead to health problems such...

  View more