BMH YAPOKEA GARI NYINGINE YA KUBEBEA WAGONJWA
BMH YAPOKEA GARI NYINGINE YA KUBEBEA WAGONJWA

Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) imepokea gari nyingine ya kubebea wagonjwa hivyo kufikisha magari hayo matatu.

Akiongea wakati wa kukabidhi gari hiyo, Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, (Mbunge wa Dodoma Mjini) amesema gari hiyo itasaidia sana kuboresha huduma za Hospitali.

"Nimshukuru Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa dhamira yake ya kuboresha huduma za afya," amesema Mhe. Mbunge.

Ndg. Mavunde ametumia fursa hiyo kuipongeza Hospitali kwa huduma nzuri inayoongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali, Dkt Alphonce Chandika.

"Hospitali hii inahudumia si wananchi wa Dodoma bali watanzania wote na tunapokea sifa nyingi kuhusu huduma zenu,"

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali, Dkt Alphonce Chandika, anasema gari hii mpya ya wagonjwa inaweza kuhimili 'rough road' hivyo kupanua wigo wa kuhudumia wananchi.

"Sasa tunaweza kuhudumia wananchi katika mazingira yoyote hivyo kupanua wigo wa kuhudumia," amesema.

Akiongea kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma (RAS), Ndg Kaspar Muya, amesema gari hii wa wagonjwa ni mkombozi wa vifo vya mama na mtoto.

"Hii gari ya wagonjwa inagusa moja kwa moja wananchi," amesema RAS.

Dondoo za Afya na Habari
Kula Mlo Kamili
Kula Mlo Kamili

Eat a combination of different foods, including fruit, vegetables, legumes, nuts and whole grains. A...

  View more
Usivute Sigara
Usivute Sigara

Uvutaji wa sigara ni hatari kwa afya ya mapafu yako, uvutaji wa sigara unaweza sababisha matatizo ya...

  View more
Punguza Vyakula vyenye mafuta mafuta
Punguza Vyakula vyenye mafuta mafuta

Fats consumed should be less than 30% of your total energy intake. This will help prevent unhealthy...

  View more
Kuendesha Gari.
Kuendesha Gari.

Unashauriwa kutokuendesha gari kila siku na wakati mwingine unatakiwa kutembea walau miguu yako na m...

  View more
Epuka ulevi wa Pombe
Epuka ulevi wa Pombe

There is no safe level for drinking alcohol. Consuming alcohol can lead to health problems such...

  View more