Mwanzo / Huduma Zetu / PROF. MAKUBI ATETA NA MADAKTARI BINGWA WA JUU WA BMH NA UDOM

PROF. MAKUBI ATETA NA MADAKTARI BINGWA WA JUU WA BMH NA UDOM

Published on April 28, 2025

Article cover image

Na Jeremiah Mbwambo, 28/04/2025 Dodoma 

PROF. ABEL MAKUBI MKURUGENZI MTENDAJI AZUNGUMZIA.
1. HUDUMA ZA HOSPITALI 
2. MAPATO YA HOSPITALI 
3. UWAJIBIKAJI NA MAADILI YA MADAKTARI BINGWA 

Tulikutana hapa mwaka jana  natukakubaliana baadhi ya mambo ambayo tumeendelea kuyaboresha na kuleta matokeo mazuri kwa Taasisi yetu na kwa wagonjwa. 

"Kwa kweli katika kuendelea kuboresha huduma niwapongeze tumeendelea kufanya vizuri zaidi hadi tumetambuliwa na Wizara ya Afya kama Hospitali bora ya kanda  inayotoa huduma bora kwa Wananchi, hongereni sana , alisema Prof. Makubi 

Ameongeza kuwa uwajibikaji na maadili kwa madaktari Bingwa ni kiapo chetu katika kuwahudumia wagonjwa, hatupaswi hata kuhisiwa vibaya juu ya mwenendo wetu 

"Katika matibabu wapo wenzetu wachache wanao weka dosari na wakati mwingine tukahisiwa vibaya kwababu ya kutokuwa makini, kwa mfano Daktari Bingwa anaweka list kubwa ya kuwahudumia wagonjwa halafu baadae anawaacha wengine au anasema muda umeisha  na kuahirisha huduma hii inaleta hisia mbaya kwa wagonjwa, wote mnafahamu huwezi kumuacha mgonjwa wakati amefika kwako hivyo ninawataka wote kukumbuka wajibu wetu na kiapo chetu mgonjwa akifika kwako na ukamuweka kwenye list basi muhudumie" alisema Prof. Makubi 

Prof Makubi amewaomba madaktari huo kujitoa zaidi kwa ajili ya huduma bora kwa Wananchi , kuongeza ubunifu wa huduma za kisasa na kuwasimamia wenzao pamoja na Wanafunzi. 

Kwa upande wake CPA. Ambele Msika Mkurugenzi wa Mipango na Fedha ameeleza kila mtumishi anatakiwa kuisaidia Hospitali kupunguza matumizi yasiyo ya lazima. 

"Nimuhimu wote kwa umoja wetu kutunza vifaa vya matibabu ili vidumu,pia kuzima taa muda usio hitajika na kufunga maji ili kuondoa bili kubwa" alisema CPA. Mssika.