WATOTO WANNE WALIOPANDIKIZWA ULOTO BMH WAMEPONA KABISA SIKOSELI-UMMY
WATOTO WANNE WALIOPANDIKIZWA ULOTO BMH WAMEPONA KABISA SIKOSELI-UMMY

Watoto wanne waliopandikizwa uloto katika Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) wamepona kabisa ugonjwa wa sikoseli, amesema Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu.

Akiwasilisha bajeti ya Wizara ya Afya kwa mwaka wa Fedha wa 2024-2025 mapema leo bungeni, Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu, amesema vipimo vimethibisha kuwa watoto hao wanne ambao ni wa kwanza kupandikizwa uloto BMH wamepona kabisa sikoseli.

"Watoto wanne (4) waliopandikizwa uloto Hospitali ya Benjamin Mkapa( BMH) wamepona kabisa siko seli. Dkt Alphonce Chandika (Mkurugenzi Mtendaji wa BMH) na timu yako hongereni sana," amesema Mhe Waziri.

Upandikizaji uloto ni matibabu ya sikoseli yanayotolewa na Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) pekee katika Ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati.

Mhe. Waziri ameongeza kuwa BMH pia wameanzisha huduma ya upandikizaji wa mimba kitaalamu IVF.

"Hivyo, wakina mama wenye changamoto ya kubeba mimba sasa suluhisho limepatikana," amesema Mhe Waziri.

Dondoo za Afya na Habari
Kula Mlo Kamili
Kula Mlo Kamili

Eat a combination of different foods, including fruit, vegetables, legumes, nuts and whole grains. A...

  View more
Usivute Sigara
Usivute Sigara

Uvutaji wa sigara ni hatari kwa afya ya mapafu yako, uvutaji wa sigara unaweza sababisha matatizo ya...

  View more
Punguza Vyakula vyenye mafuta mafuta
Punguza Vyakula vyenye mafuta mafuta

Fats consumed should be less than 30% of your total energy intake. This will help prevent unhealthy...

  View more
Kuendesha Gari.
Kuendesha Gari.

Unashauriwa kutokuendesha gari kila siku na wakati mwingine unatakiwa kutembea walau miguu yako na m...

  View more
Epuka ulevi wa Pombe
Epuka ulevi wa Pombe

There is no safe level for drinking alcohol. Consuming alcohol can lead to health problems such...

  View more