TUNAHITAJI MASHIRIKIANO NA TAASISI NYINGINE ILI KUTIMIZA DIRA YA HOSPITALI YA BENJAMIN MKAPA

Published: Jan 06, 2026
TUNAHITAJI MASHIRIKIANO NA TAASISI NYINGINE ILI KUTIMIZA DIRA YA HOSPITALI YA BENJAMIN MKAPA cover image

Na. Jeremiah Mbwambo, 06/01/2026 Dodoma 

Picha: Ludovick Kazoka 

 

Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi Mtendaji Hospitali ya Benjamin Mkapa Prof. Abel Makubi wakati akifungua kikao cha kutathimini hati zote za makubaliano ambazo Hospitali ya Benjamin Mkapa imeingia na Taasisi nyingine. 

 

"Mimi ninaamini mashirikiano mazuri na Taasisi nyingine yanaweza kutufanikisha kufikia dira, peke yetu hatuwezi kufikia" amesema Prof. Makubi 

 

Ameongeza kuwa ni muhimu kuwa wa wazi kabla au baada ya kuingia kwenye kusaini hati ya makubaliano 

 

"Tunaposaini hati za makubaliano ni muhimu kutekeleza maana makubaliano yoyote yana pande mbili, ikiwa hayatekelezeki tuseme tusikae kimya" amesema Prof. Makubi 

 

Tathimini hii ya hati za makubaliano ni hatua muhimu ya Hospitali ya Benjamin Mkapa kuimarisha huduma zake kupitia wadau wake.