Huduma ya Upandikizaji Uroto
Published on June 18, 2025

Idara ya Hematologia – Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH)
Kinara wa Huduma za Magonjwa ya Damu Afrika Mashariki na Kati
Utangulizi
Idara ya Hematologia ya Hospitali ya Benjamin Mkapa ni kitovu cha kitaifa na kikanda cha huduma maalum za magonjwa ya damu. Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2018, idara imeendelea kukuza uwezo wake kitaaluma na kiteknolojia, na mwaka 2022 ikajitegemea rasmi kutoka Idara ya Magonjwa ya Ndani.
Lengo kuu la idara ni kutoa huduma za utambuzi, matibabu na usimamizi wa magonjwa ya damu, yakiwemo magonjwa ya kurithi kama vile selimundu (sickle cell anemia), pamoja na magonjwa ya saratani ya damu.
Mafanikio ya Mwaka 2023
- Idadi ya Wagonjwa: Takribani wagonjwa 5,000 walihudumiwa.
- Taratibu Maalum: Zaidi ya 100 zilitolewa, ikiwa ni pamoja na utoaji damu wa hali ya juu na huduma za upandikizaji wa uboho wa mifupa (BMT).
- Huduma ya BMT: Ilianzishwa rasmi kwa wagonjwa wa selimundu, ikiwa ni ya kwanza kutolewa Afrika Mashariki na Kati. Wagonjwa 21 walifanyiwa upandikizaji kwa mafanikio makubwa.
Huduma Zinazotolewa
1. Utambuzi na Matibabu
- Magonjwa Yasiyo ya Saratani (Benign):
ü Anemia mbalimbali
ü Trombositopenia ya kinga
ü Aplastic anemia
ü Thalassemia na selimundu
ü Hemophilia, DVT, PE
- Magonjwa ya Saratani ya Damu (Malignant):
ü Leukemia
ü Lymphoma
ü Myeloma
ü Myelodysplastic syndromes
ü Myeloproliferative neoplasms
2. Vipimo vya Utambuzi
- Peripheral Blood Smear
- Bone Marrow Morphology & Trephine Biopsy
3. Huduma za Damu
- Automated RBC exchange
- Apheresis (utoaji wa sahani damu)
- Phenotyping ya kinga ya seli nyekundu
Muundo wa Idara
1. Kliniki ya Wagonjwa wa Nje
- Ushauri wa hematologia ya jumla
- Ufuatiliaji baada ya BMT
- Huduma kwa wagonjwa wa hemoglobinopathies (mfano selimundu)
- Huduma za oncology na hematologia nyingine
2. Kitengo cha Wagonjwa wa Kulazwa
- Huduma za karibu kwa wagonjwa mahututi
- Ziara za kitabibu hufanyika kila baada ya siku mbili
3. Kitengo cha BMT
- Upandikizaji wa uboho kwa wagonjwa wa selimundu kutoka kwa ndugu waliolingana
- Ushirikiano na UDOM na Wizara ya Afya kuanzisha Kituo cha Umahiri cha Kikanda
4. Maabara ya Hematologia na Benki ya Damu
- Huduma za vipimo vya damu na usimamizi wa transfusion
Wafanyakazi na Utaalamu
- Madaktari Bingwa:
ü 2 Hematologists
ü 1 Pediatric Hemato-Oncologist
- Madaktari wa Tiba ya Jumla: 3
- Wauguzi:
ü 4 waliobobea katika huduma za BMT
ü 6 wauguzi wa kawaida
ü 1 muuguzi wa anticoagulation
- Wafamasia:
ü 2 wa kliniki
ü 5 wa kawaida
Ushirikiano wa Kisekta
Idara inashirikiana na wataalamu wa lishe, wanasaikolojia, mazoezi ya viungo, na wafanyakazi wa kijamii. Pia ina ushirikiano wa kitaaluma na wataalamu kutoka Italia kwa ajili ya huduma za BMT.
Mafanikio Makuu
- BMT kwa Wagonjwa wa Selimundu: Wagonjwa 16 walifanyiwa BMT kwa mafanikio
- Huduma ya Damu: Kuanzishwa kwa huduma ya RBC exchange
- Idadi ya Wagonjwa: Zaidi ya 5,000 huhudumiwa kila mwaka
Mikakati ya Baadaye
- Kuanzisha Kituo cha Umahiri cha Kikanda
ü Ushirikiano na UDOM & Wizara ya Afya
ü Huduma za kibingwa, tafiti, na mafunzo
- Kupanuwa Huduma za BMT
ü Kujumuisha magonjwa kama aplastic anemia na leukemia
- Elimu kwa Umma
ü Kampeni za uhamasishaji na uchunguzi, hasa vijijini
- Maendeleo ya Rasilimali Watu
ü Mafunzo ya mara kwa mara kwa madaktari na wauguzi
ü Ushiriki katika warsha za kitaifa na kimataifa